DAH HII MIMEA NI YA AJABU DUNIANI

 Kama tunavofahamu kuna aina nyingi za mimea duniani, tunazozijua na tusizozijua. Lakini katika mimea hiyo hiyo iko ambayo ina sifa za kustaajabisha kutokana na maumbile, muonekano, tabia au madhara yake.

Hapa chini ni mimea ya aina tano ambayo ni ya ajabu zaidi. Usisahau kuweka comment yako mwisho wa makala hii. 


1. MIANZI

(Mimea inayokuwa kwa haraka)

Mianzi ni miti ya jamii ya magugu ambayo muonekao wake ni kama mua. Miti hii hupatika sehemu kadhaa duniani. Kwa hapa Tanzania hupatikana sana Mkoa wa IRINGA. Pia hutumika kwa matumizi mbali mbali ikiwemo kujengea, kutengeneza vifaa vya asili kama vile kapu n.k. Lakini pia baadhi ya watu huitumia kugema pombe.

Maajabu ya mianzi ni kwamba ndio mti unaoongoza kwa kukua kwa haraka zaidi. Unaambiwa muanzi unaweza kukuwa kwa urefu wa hadi sentimeta 90 kwa siku. (Umeipata hiyo?)

Mimea ya Mianzi

2.VENUS FLYTRAP
(Mmea unaokula nyama)

Siku zote tunajua wadudu ndio hula mimea, ama sivyo? Lakini katika hili ni kinyume. Mmea huu ndio hula wadudu.

 Unajua kivipi?

Mmea huu huwanasa wadudu kwa majani yake kisha kuwafunika na kuwamengenya.

Majani ya mimea hii hufanya kama mtego. Mdudu anapotua katika jani la mmea huo jani hilo hujifunika ghafla kwa kasi ya chini ya nusu sekunde. Kisha mmea huo hutoa kemikali za kummeng'enya mdudu pole pole ndani ya siku kumi kisha hujifungua tena.

Venus Flytrap hupatikana katika maeneo ya CAROLINA huko nchini Marekani.

Venus flytrap

3. MANCHINEEL

(Mmea wenye sumu kali)

Suala la mimea kuwa na sumu sio geni, lakini kwa mmea huu ni ajabu zaidi kwani sumu yake ni kali na ya ajabu.

Mmea huo huwa na maji maji ya rangi ya maziwa ambayo humdhuru mtu akiyagusa tu. Ukigusa jani lake pia litakudhuru na kukusababishia vidonda na kuwa kama umemwagiwa maji ya moto.

Hutakiwi kujikinga na mvua chini ya mmea huu, kwani maji ya mvua yakichanganyikana na maji maji yake yakakuangukia mwilini yanaweza kukuwasha sana na kukusababishia madhara.

Lakini pia haitoshi, mmea huo ukichomwa moshi wake ni sumu kali na huweza kumtia upofu mtu na kumsababishia matatizo ya kupumua.

Muonekano wa matunda yake ni kama tunda la tufaha (apple) lakini lina sumu kali sana kiasi kwamba ukilila unaweza kupoteza maisha mara moja.

Manchineel

4. MIMOSA PUDICA
(Mmea wenye hisia)

Sitaki kuamini kama hujawahi kukutana na mmea huu. Nakumbuka nikiwa mdogo kulikuwa na majani flani hivi ukiyagusa yanasinyaa muda huo huo na baadaye kurudi kama kawaida. Sasa huu ndio mmea tunaouzungumza (Mimosa pudica)

Unaambiwa katika mmea huu hii ni njia ya kujikinga na wanyama walao nyasi na hata wadudu.  Kwani jani linaposinyaa kwa kuguswa basi mdudu anaweza kudondoka ama mnyama kuweza kuacha kula jani hilo na kuondoka.

Mimosa pudica

5. REFLESSIA ARNOLDII
(Mnuka uvundo)

Huu ndio mmea wenye maua makubwa zaidi duniani. Ua lake lina upana wa mita moja na pia hauna shina, majani wala mizizi (Unashangaza ee?)

Mmea huu bwana hupatikana sana maeneo yenye misitu ya mvua nyingi huko Sumatra na Borneo nchini Indonesia.

Mmea huu unanuka harufu ya mzoga na ni harufu kali sana.

Reflesia arnoldii


Je ni mmea gani wa ajabu ambao unaufahamu? Tuandikie maoni yako hapo chini.

1 Comments

Post a Comment

Previous Post Next Post